

Tanzania ni nchi ya amani na upendo. Ina makabila zaidi ya mia ishirini na nane.
Moja ya makabila ni Maasai ambalo ni maarufu kwa ufugaji na mavazi yao.
Kuna mbuga mbalimbali Tanzania kama vile Serengeti, Manyara, Mikumi, Saadani, Ruaha na nyingine nyingi.
Watalii wengi huvutiwa kuja kutalii.
Nchi ya Tanzania ina mito na bahari nyingi sana ambamo watu wengi na hata watoto hupenda kuogelea. Mto Ruaha ni moja ya mito mikubwa Tanzania.
Lakini, yapaswa watu kuwa waangalifu kwani mito mingine ni hatari kwa sababu kuna wanyama hatari kama mamba na viboko.
Wanyama mbalimbali wanapatikana katika nchi hii nzuri. Wanyama hawa ni kama simba, tembo, nyati, swala, pundamilia, chui, fisi na wengineo.
Hata ndege mbalimbali hupatikana katika nchi hii iliyobarikiwa.
Watu wa makabila na dini mbalimbali, huishi pamoja kwa amani na upendo.
Hakuna dini, ukabila, wala ubaguzi wa aina yoyote. Ukifika Tanzania, jua umefika nyumbani.
Watu wa Tanzania ni wakarimu sana hata kwa wageni. Upendo na ukarimu ndio jadi yetu.
Ukarimu, uzalendo na upendo vinaifanya Tanzania iwe nchi yenye nuru sana.
Mlima mrefu katika bara la Afrika, Mlima Kilimanjaro, hupatikana nchini Tanzania. Tunajivunia kuwa na mlima mrefu zaidi Afrika.
Pia, kuna milima mingi sana nchini humu na viziwa tele hasa Zanzibar.
Biashara, uwekezaji, uvuvi, kilimo, uchimbaji madini na utalii ni mojawapo ya shughuli mbalimbali za kufanya nchini Tanzania.
Utalii una mchango mkubwa kwenye maendeleo ya nchi yetu. Watanzania wengi pia hujishughulisha na biashara.
Raisi wa Tanzania ni Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Huyu ndiye mwanamke wa kwanza kuongoza kama Raisi katika nchi ya Tanzania.
Watoto wote wanatakiwa kusoma kwa bidii ili wapate viongozi waadilifu wengi na mabolozi wazuri wa nchi yetu. Kwani nchi yetu ina utajiri mwingi tena wa asili.
Nchi yetu inavutia, ni yenye nuru na tunu kubwa kwa Watanzania. Wanawake na wanaume wote wana wajibu katika nchi hii.
Wanawake wanaweza, kwa hivyo sote tuendelee kuchapa kazi kwa bidii. Tuna mchango mkubwa sana kwa nchi hii. Sote tunatakiwa kuilinda nchi yetu na kuwa wazalendo kwa ajili ya leo na kesho yetu sote.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu wabariki watanzania

