Shamba Langu
Rumba Bro
Kenneth Boyowa Okitikpi

Mimi naitwa Amina. Wazazi wangu walinipa sehemu ndogo ya shamba ambayo nilitumia kupanda maua.

1

Kila asubuhi natembelea shamba langu kumwagilia maua maji na kutoa magugu.

2

Siku moja niliamua kwenda kumtembelea nyanyangu. Nilienda shambani kuchuma maua. Nilitaka kumpa shada la maua kutoka bustani yangu. Nilipokuwa nachuna maua, niligundua mawingu yameanza kubadilika kana kwamba mvua ingenyesha.

3

Baada ya umeme kupiga, papo hapo palitokea mngurumo na radi ikawa ishara tosha kuwa mvua kubwa ingenyesha.

4

Wazo lilinijia nikimbie nyumbani kabla mvua kunipata. Mara baada ya wazo hilo, kulianza kunyesha na maji ikalowa kwenye ardhi. Niliteleza na kuanguka chini pu!

5

Nilipoinuka, nilihisi uchungu mwingi. Niligundua kuwa nimeumia mgongo na paji la uso. Mara familia yangu ilinipeleka hospitalini.

6

Pale hospitalini madaktari walinitibu na kuniitunza vyema. Familia yangu pia walinitembelea na kuniiletea maua kutoka kwenye shamba langu ili kunitia moyo niweze kupata nafuu haraka.

7

Baada ya kukaa hospitalini wiki nzima nilipata nafuu. Daktari aliniruhusu kutoka hospitalini. Wazazi wangu walipokuja kunichukua, muuguzi alinipa dawa ninywe nyumbani. Nilifurahi sana kurudi kwetu.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Shamba Langu
Author - Rumba Bro
Illustration - Kenneth Boyowa Okitikpi, Jesse Breytenbach
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs