

Hapo zamani za kale, palitokea mwanamke aliyekuwa amebeba kikapu mawele kikapuni.
Pia, alikuwa na fimbo yake kubwa.
Siku moja Sungura alikuwa na njaa sana. Hakuwa na chakula wala shamba. Alikuwa amekonda sana.
Sungura huyo alikuwa mvivu. Hakuweza kulima, hakuweza kupanda mimea, hakuweza kupalilia. Sungura alitaka chakula, lakini, hakujua afanyeje.
Ilibidi akaenda kwa mwanamke akamwambia, "Mimi nina shamba kubwa la mawele." Kumbe Sungura ni mjanja.
Alienda kwenye shamba la wenyewe kisha akamwambia mwanamke, "Hili ndilo shamba langu."
Yule mwanamke akachuma mawele yale ya wenyewe.
Sungura akamuona mwenye shamba la mawele anakuja. Akakimbia na kumuacha huyo mwanamke.
Yule mwanamke hakumuona mwenye shamba akija. Alipofika, alimwuliza, "Nani kakuruhusu uchume mawele yangu?"
Mwanamke akamjibu, "Sungura ameniambia ni shamba lake na akaniambia nichume mawele yake."
Mwenye shamba akamwuliza, "Huyo sungura yuko wapi?"
Mwanamke akamwambia, "Alikuwa amejificha hapa. Sasa yuko wapi?"
Wakamtafuta Sungura bila kufanikiwa kumpata.
Ndio mpaka leo sungura na mwanadamu hawapatani.

