Binadamu wa ajabu
Honorata Akaro
Honorata Akaro

Hapo zamani za kale, palikuwa na mwanamume aliyeitwa Kijogoo.

Kijogoo alikuwa mrefu sana.

1

Watu walizoea kusema, "Huyu ni binadamu wa ajabu!"

Alipokuwa mdogo, mama yake na baba yake walimpeleka kwa mganga.

2

Mganga aliwaambia, "Mtoto huyu amepewa laana. Baada ya kumzaa hamkumpa baraka zake. Kwa hivyo atakuwa na miguu mirefu. Na atakapofikia jua, atakufa!"

3

Mama na baba walishangaa.

Baba akamlaumu mama akisema, "Wewe ndiye umesababisha maafa haya. Hukumpa baraka Kijogoo kwa kutoa sadaka ya ng'ombe dume na jike."

4

Kijogoo aliteseka.

Alipofikia jua, alifariki.

5
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Binadamu wa ajabu
Author - Honorata Akaro
Illustration - Honorata Akaro
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs