Mzee anaenda kuwinda
Kelvin Urono
Jacob Kono

Siku moja, mzee mmoja alikwenda porini.

Alitaka kuangalia mtego wake kwa lengo la kupata chakula.

1

Alipokaribia, aliona twiga amenaswa kwenye mtego wake.

Alifurahi sana.

2

Aliwaza akasema moyoni, "Nikimfungulia yule twiga atakimbia."

Alibadilisha mawazo akaamini kuwa twiga hangeondoka.

Aliwaza, "Nikimfungulia yule twiga nitaweza kumuua."

3

Akarusha mkuki na kwa bahati mbaya akakata kamba badala ya kumuua twiga.

Alihuzunika sana.

4

Kwa hasira, alimrukia yule twiga. Akashika mkia wake akiwa anajua kuwa twiga atadondoka.

Twiga yule alikazana na kukimbia.

5

Twiga akampiga yule mzee teke la tumbo.

Mzee akadondoka chini.

6

Mzee akaelekea kwake kwa maumivu bila chakula chochote.

Alilalamika sana.

7
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mzee anaenda kuwinda
Author - Kelvin Urono
Illustration - Jacob Kono
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs