

Hapo zamani za kale, palikuwa na mwanamume aliyeitwa Omar.
Omar alikuwa na mke wake aliyeitwa Rachel.
Omar alikuwa akimlaumu mke wake kuwa hawezi kuzaa.
Hivyo aliamua kuoa mara ya pili.
Alimuoa mwanamke aliyeitwa Katia.
Katia alifanikiwa kupata mtoto aliyeitwa Michael.
Mzee Omar alipompata mtoto wa kiume, alimdharau mke wake wa kwanza, Rachel.
Rachel alijisikia vibaya na akataka kujiua. Mfanyakazi mmoja akasema, "Mkubwa wangu, usifanye hivyo!"
Miaka 10 baadaye, Rachel alimpata mtoto wa kike aliyeitwa Rosita.
Rosita alipofikisha miaka 5, alikuwa na sauti nyororo.
Hata hivyo, baba yake alimfungia na kumwambia, "Hauna sauti ya kuimba nyimbo zozote!" Rosita alisikitika sana.
Baada ya miaka 5, Rachel aliugua na mwishowe akafariki.
Rosita alilia sana.
Siku moja, Rosita alisikia kuwa kutakuwa na mashindano ya kuimba. Aliandaa rinda jeupe. Alipendeza sana.
Siku iliyofuata, Rosita alijiunga na waimbaji wengine. Alisubiri, na alipoitwa, aliimba wimbo ufuatao:
Lily alikuwa msichana mdogo, alihofia ulimwengu mkubwa, mpana. Alilelewa ndani ya kuta za ngome. Mara kwa mara alijaribu kukimbia. Na kisha usiku na jua kutua, alikwenda msituni. Akiwa na hofu sana, kwa kuwa peke yake!
Baba yake alisikia sauti nzuri ya binti yake.
Alimuomba binti yake msamaha huku akilia na kusema, "Kuanzia leo nitakuruhusu kuimba nyimbo mbalimbali."

