Milango Ya Fahamu
Ubongo
Ubongo

Kuna milango mitano ya fahamu: macho, masikio, pua, ulimi na vidole.

1

Ninatumia macho yangu kuona.

2

Naweza kuona paka.

Naweza kuona panya.

3

Ninatumia masikio yangu kusikia.

4

Naweza kusikia sauti ya basi. 

Beep! Beep!

Naweza kusikia sauti ya gari.

Vroom! Vroom!

5

Ninatumia pua yangu kunusa.

6

Naweza kunusa maua.

Naweza kunusa chakula.

7

Ninatumia ulimi wangu kuonja.

8

Naweza kuonja ndizi tamu.

Naweza kuonja supu ya chumvi.

9

Ninatumia vidole vyangu kugusa.

10

Naweza kugusa blanketi laini.

11

Naweza kugusu kitabu kigumu.

12

Kuna milango mitano ya fahamu: macho, masikio, pua, ulimi na vidole.

13

Milango mitano ya fahamu inanisaidia kufahamu mazingira yangu.

14
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Milango Ya Fahamu
Author - Ubongo
Illustration - Ubongo
Language - Kiswahili
Level - First sentences