Siku za wiki
Ubongo
Ubongo

Kila wiki ina siku saba:

Jumatatu, Jumanne, Jumatano, Alhamisi, Ijumaa, Jumamosi na Jumapili.

1

Siku ninayoipenda ni Jumatatu. Ni siku ya kwanza ya wiki.

Huwa ninaenda shule siku ya Jumatatu.

2

Jumanne ni siku ya pili ya wiki.

Inafuata baada ya Jumatatu.

3

Jumanne huwa tunacheza michezo tunayoipenda shuleni.

4

Jumatano ni siku ya tatu ya wiki.

Iko katikati ya wiki.

5

Siku ya Jumatano huwa tunapaka rangi shuleni.

6

Baada ya Jumatano inafuata Alhamisi.

Alhamisi ni siku ya nne ya wiki.

7

Watoto wakubwa hutusimulia hadithi siku ya Alhamisi.

8

Ijumaa ni siku ya tano ya wiki.

Ijumaa ni siku ya mwisho ya wiki kwenda shule.

9

Tunapenda kula sambusa siku ya Ijumaa.

10

Mchana, tukifika nyumbani huwa tunajitayarisha kwa wikiendi kuanza.

11

Jumamosi ni siku ya sita ya wiki.

12

Siku ya Jumamosi huwa tunaangalia katuni...

13

...na kwenda sokoni.

14

Jumamosi na Jumapili ni siku za kucheza na kupumzika.

15

Jumamosi huwa tunaenda sokoni kununua matunda ninayoyapenda sana.

16

Jumapili ni siku ya mwisho ya wiki. Ni siku ya mapumziko kabla ya kuanza wiki mpya.

Jioni huwa ninaandaa vifaa vyangu vya shule.

17

Wiki ina siku saba:

Jumatatu, Jumanne, Jumatano, Alhamisi, Ijumaa, Jumamosi na Jumapili.

18
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Siku za wiki
Author - Ubongo
Illustration - Ubongo
Language - Kiswahili
Level - First sentences