Ratiba ya mama yangu
Njeri Wachira

Mama yangu anapoamka, hutandika kitanda chake kwanza.

1

Huingia jikoni kutayarisha kiamsha kinywa. Pia, hutayarisha vitafunio na kuviweka ndani ya mifuko midogo.

Wanawe hula vitafunio hivi wakati wa mapumziko ya saa nne na saa sita.

2

Kiamusha kinywa huwa ni uji wa nafaka, chai na mkate, maji ya machungwa au maziwa.

3

Huwaamsha wanawe na kuwaelekeza wapige mswaki, wanawa nyuso na kuvaa sare za shule.

4

Familia yake inapomaliza kujitayarisha, huelekea mezani kula kiamsha kinywa.

5

Baba huenda zake.

Mama huwaingiza wanawe kwenye gari lake na kuwapeleka shule.

6

Huwapungia mkono watoto na kuwambia, "Kwaherini, tuonane jioni."

7

Huliendesha gari lake mpaka kituo cha gari la moshi.

8

Huingia kwenye gari la moshi na kuelekea mjini anapofanya kazi ya uhasibu.

9

Saa kumi zinapofika, mama huiacha kazi yake haraka.

Yeye hurudi kwenye kituo cha gari la moshi.

10

Huingia na kuelekea nyumbani.

Inapofika saa kumi unusu kamili, huwachukua watoto wake waende nyumbani.

11

Watoto huwa wamemngoja kwa hamu.

Wao huingia kwenye gari haraka wakilia njaa.

12

Wanapofika mlangoni, watoto hutimua mbio ili wakale mkate uliobaki.

13

Mama huanza kupika chakula cha jioni na kuwaandalia wanawe.

Wanapomaliza, wote huwa wamechoka kweli.

14

Lakini bado vyombo havijaoshwa.

Je, ni nani atakayeviosha vyombo?

15
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Ratiba ya mama yangu
Author - Njeri Wachira
Illustration -
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs