

Nilipokuwa mtoto mdogo, tuliishi katika shamba moja pamoja na wazazi wangu na ndugu zangu.
Nilipenda kuwatazama wadudu wakifanya kazi zao.
Wadudu niliopenda kuwatazama zaidi ni buibui.
Waliishi mahali mbalimbali katika boma letu.
Nilitumia muda mwingi nikiwatazama na kuona waliyokuwa wakifanya.
Nilipojua kusoma, nilifanya utafiti katika vitabu na kujua mambo mengi sana kuwahusu.
Nilijifunza kwamba miili yao ina sehemu mbili tu, ambazo ni kichwa na tumbo.
Buibui huwinda na kushika mawindo.
Wengi huwinda wadudu wengine.
Pia nilijifunza kwamba buibui wana sumu.
Wao hutumiwa sumu hiyo kuua mawindo yao.
Kabla ya buibui kula chakula chake, lazima akifanye kiwe majimaji.
Hutengeneza hariri ambayo huitumia kujenga nyumba yake iitwayo utando.
Hutaga mayai mengi na huyalinda kwa kutumia utando wake.
Buibui wengi wana miguu minane ambayo hutumika kutembea na kupanda.
Buibui wengine wana macho manane na wengine wana sita.
Ajabu!
Nilitamani sana kumweka buibui mmoja kama mnyama kipenzi.
Hata hiyvo, mama yangu alikataa kata kata.

