Dereva Juma
Jemimah Makena

Juma anaishi mjini.

Yeye ni Dereva wa gari la abiria.

1

Juma ni dereva stadi na mwenye heshima kwa wateja wake.

2

Siku moja, Kasim, ambaye alikuwa jirani yake alimpa kazi.

Alitaka Juma awaendea wageni wake kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Moi. Wageni walikuwa wakitoka ng'ambo.

3

Kasim pia alimwambia awatafutie wageni wake hoteli safi na yenye mandhari ya kuvutia.

4

Wageni walipofika hotelini, waliagiza samaki.

Walimwalika Juma kushiriki nao chakula cha mchana.

Kasim pia alijiunga nao.

5

Alasiri siku hiyo, Kasim aliwapeleka wageni wake kwenye Mbuga ya Wanyama.

6

Juma alitaka sana kufika mapema kabla ya lango la Mbuga kufungwa.

Ilimbidi aliendeshe gari lake kwa kasi sana.

7

Askari waliokuwa zamu wakaliona gari lake Juma likipita kasi.

8

Mgeni mmoja akaamka kutoka usingizi wa pono na kufoka kwa sauti kubwa, "Taratibu dereva! Utasababisha ajali."

9

Gari la polisi lililokuwa linawafuata likawafikia.

Inspeka wa polisi akawaamurisha washuke chini.

10

Juma alijitetea, lakini wapi! Alikuwa amevunja sheria za barabarani.

Waliandamana mpaka kituo cha polisi.

11

Juma alitozwa faini na akaomba mshamaa. Askari wakamrejeshea gari lake.

Kasim akaomba msamaha kwa wageni wake. Wakaanza safari tena kuelekea Mbugani.

12

Walifika Mbugani saa kumi na mbili unusu. Lango la Mbuga lilikuwa halijafunguliwa.

Juma aliwaomba wageni wa Kasim msamaha.

Tangu siku hiyo, Juma huliendesha gari lake kwa kuzingatia sheria za barabarani.

13
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Dereva Juma
Author - Jemimah Makena
Illustration -
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs