

Hapo zamani, Sima na Samaki waliishi katika kijiji kimoja.
Urafiki ulianza kati yao.
Samaki alimwambia rafiki yake Sima waende pamoja baharini waogelee.
Walishika njia wakaenda baharini.
Walipofika kando ya bahari, Samaki alimwambia Sima, "Mimi naingia majini kuoga," kisha akapiga mbizi.
Baada ya kuogelea kwa muda mfupi, Samaki alimwambia Sima, "Sasa ni zamu yako kuogelea."
Sima alimjibu, "Siwezi kuogelea. Nikiingia majini, nitazama halafu nitaumbuka."
Samaki alimbembeleza Sima akisema, "Njoo ujaribu. Hutaumbuka na ukizama, nitakuokoa." Sima alikubali.
Sima alipofika majini, alishindwa kuelea. Alimwita Samaki, "Njoo uniokoe," lakini Samaki hakumwokoa.
Mtu mmoja alimsikia Samaki akilalamika kwamba hangeweza kumwoka Sima. Mtu huyo akamwuliza, "Kuna shida gani?"
Samaki akasema, "Huyu mjinga ameingia majini na sasa anazama." Mtu huyo alimwokoa Sima.
Sima alipotoka majini, alisema, "Samaki ni rafiki mbaya. Amenishawishi niogelee nami sijui kuogelea."
Mtu huyo aliwaambia, "Hebu niwatatulie tatizo hili." Alikata Sima na Samaki, akala kwa fujo. Na huo ukawa mwisho wa ugomvi kati yao.

