Anayenipenda, hujua ninachopenda
Palmesi Katangambo
Natalie Propa

Hapo zamani za kale, palikuwa na mfalme.

Yeye na wake zake watatu, waliishi katika kijiji kimoja kilichoitwa Nuru.

1

Siku moja, mfalme yule aliwaita wake zake na kusema, "Wake zangu wapendwa, ningependa leo nile chakula kitamu. Atakayepika chakula kitamu zaidi, atapata zawadi nono."

2

Mke mmoja alienda sokoni akanunua nyama ya ng'ombe na viungo vingi.

Alirudi nyumbani na kupika kitoweo alichoamini kilikuwa kitamu.

3

Mke mwingine alienda soko iliyokuwa sehemu tofauti. Alinunua nyama ya pori pamoja na viungo tofauti.

Naye alirudi nyumbani kuitayarisha.

4

Mke wa mwisho aliamua kwenda kumuona mamake mfalme.

Aliambiwa apike chakula cha kienyeji na wala asiweke mafuta au viungo vyovyote vya kisasa.

5

Mke huyo wa tatu, alienda shambani kutafuta mboga tofauti za kutayarishia chakula cha kienyeji.

6

Mfalme na wenzake walifika kwa wake waliopika nyama ya ng'ombe na ya pori. Hata hivyo, mfalme hakukipenda chakula alichoandaliwa.

Walienda kwa mke aliyeandaa chakula cha kienyeji.

7

Mfalme alikifurahia sana kwani kilikuwa chakula alichokipenda. Alimteua mke huyo kuwa malkia katika ufalme wake.

Tangu siku hiyo, huyo mke aliheshimiwa sana. Yeye alijua namna ya kumfurahisha mmewe.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Anayenipenda, hujua ninachopenda
Author - Palmesi Katangambo
Illustration - Natalie Propa, Rob Owen, Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs