Akili ni mali
Ursula Nafula
Abraham Muzee

Sokwe alimkuta Mamba kando ya mto mkubwa.

1

Mamba akasema, "Nina maumivu. Tafadhali nisaidie."

2

Sokwe akamwuliza, "Unahitaji nini?"

3

Mamba akamjibu, "Usiponipatia moyo wako, sitapona."

4

Sokwe akasema, "Kwanza nibebe hadi upande wa pili wa mto."

5

Mamba akambeba Sokwe mgongoni wakavuka mto.

6

Sokwe akasema, "Ninahitaji kisu ili niukate moyo wangu."

7

Wakati huo huo, upepo mkali ukaanza kuvuma.

8

Mamba akainuliwa juu karibu amuangushe Sokwe.

9

Sokwe alipoiona nchi kavu, akamwambia Mamba aharakishe.

10

Ghafla, Sokwe akaurukia mti.

11

Mamba akakasirika akasema, "Ulinidanganya! Utajuta!"

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Akili ni mali
Author - Ursula Nafula
Illustration - Abraham Muzee
Language - Kiswahili
Level - First words