Akadeli abahatika
Simon Ipoo
Rob Owen

Siku moja Akadeli, Lucia, Acharait na Maria walienda msituni kutafuta matunda.

Walishikana mikono wakavuka mto mkubwa.

1

Waliufikia mti uliojaa matunda mabivu. Walikubaliana kuukwea mti ule kuyachuma matunda.

Sharti lilikuwa wayafumbe macho yao wakifanya hivyo.

2

Hata hivyo, Lucia, Acharait na Maria hawakuyafumba macho yao.

Akadeli pekee alifanya hivyo alipokuwa akichuma matunda.

3

Ilipofika wakati wa kuyafumbua macho, Akadeli alikuta kwamba alikuwa ameyachuma matunda mabichi pekee.

4

Lucia, Acharait na Maria walimcheka Akadeli kisha wakaondoka kwenda zao nyumbani.

Akadeli aliyatupa matunda yale mabichi akaanza kuchuma mabivu.

5

Muda mfupi baadaye, Akadeli alikijaza kikapu chake kwa matudna mabivu.

Alianza kuuvuka mto ule mkubwa peke yake.

6

Akadeli alipokuwa katikati, kikapu chake kilimponyoka na kuanguka majini.

Alikasirika sana akaanza kulia.

7

Kabla hajavuka ng'ambo, Akadeli alimwona samaki ukingoni mwa mto.

Alimchukua.

8

Alipokuwa amembeba samaki yule, mwewe alimnyang'anya akaruka naye juu.

9

Akadeli aliona unyoya mmoja mrefu uliokuwa umeachwa na mwewe.

Ingawa alikasirika, aliuchukua ule unyoya na kuendelea na safari yake.

10

Akadeli aliwapita watu wakisherehekea harusi ya kitamaduni.

Wachezaji walivalia nyasi vichwani badala ya manyoya kama ilivyokuwa desturi.

Waliuchukua ule unyoya wakampatia fahali mkubwa!

11

Akadeli alifika nyumbani na fahali wake. Wazazi na jamaa zake walifurahi sana.

Lucia, Acharait na Maria walisikitaka kumdanganya Akadeli. Ilikuwa siku ya bahati kwa Akadeli!

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Akadeli abahatika
Author - Simon Ipoo
Illustration - Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs