

Jina langu ni Kobole.
Ninaishi katika kijiji kiitwacho Mbalisana.
Siku moja nilikuwa nikichuma matunda.
Nilishuhudia jambo la kushangaza.
Niliona mistari ya rangi tofauti angani.
Niliyaangusha matunda niliyokuwa nimechuma.
Kisha, nikakimbia kuwaambia watu nyumbani.
Niliwapata wakiwa nje.
Wote walitazama juu kwa mshangao.
Nilisema kwa furaha, "Hii ni shuka maridadi."
Neno alinipinga akisema, "La! Hizi ni rangi tofauti zinamwagika kutoka angani."
Baadhi ya wanakijiji walikubaliana nami na wengine waliamini aliyosema Neno.
Tulianza kubishana.
Wakati huo, mgeni mmoja alitokea na kusema, "Mmekosea nyote."
Tulipiga mayowe, "Ikiwa tumekosea, wewe tueleze ukweli."
Yule mgeni alisema, "Mnachoshuhudia ni upinde. Kwani ninyi hamjawahi kuuona upinde?"
Kwa mshangao zaidi, tulimjibu, "La! U-p-i-n-d-e ni nini?"
Neno alimwuliza, "Je, huu upinde ni wetu? Tunaweza kuuweka hapa?"
Hatukupata majibu kwa maswali yetu. Mgeni huyo alikuwa tayari ameenda zake.

