Mhogo na Mtende
Divine Apedo
Brian Wambi

Hapo zamani, Mhogo na Mtende waliishi kijijini Koowa. Kama marafiki, walitembeleana kila siku.

Walikuwa wakulima waliofanya kazi kwa bidii katika mashamba yao.

1

Katika mwaka mmoja, kulikuwa na ukosefu wa mvua. Mimea yote ilikauka. Watu wakakosa chakula.

Mhogo na Mtende waliamua kwenda kutafuta kazi katika kijiji tofauti.

2

Wlimkuta mwanamke mmoja wakamsalimu, "Hujambo?" Aliitikia kisha akwauliza, "Mnakwenda wapi?"

Mtende alimjibu, "Tunakwenda kutafuta kazi katika kijiji jirani."

3

"Kazi gani mnayofanya?" Mwanamke yule aliuliza. Walijibu, "Tunaweza kuipa chakula familia yako na mifugo wako.

Mwanamke alwauliza tena, "Mtahitaji nini kutupatia chakula hicho?" Walimjibu, "Tupe ardhi, maji na huduma nzuri."

4

Mwanamke yule aliwapeleka nyumbani kwake.

5

Alasiri moja, Mtende na Mhogo walibishana vikali. Mhogo alisema kuwa yeye alikuwa muhimu zaidi kuliko Mtende.

Mtende naye akasema kuwa yeye alikuwa muhimu kuliko Mhogo.

6

Mwanamke yule aliwasikia kutoka chumbani kwake.

Alitoka nje na kwauliza, "Mbona mnabishana?"

7

Mhogo alikuwa wa kwanza kuzungumza. "Mimi ni muhimu zaidi kuliko Mtende. Ninazaa mihogo mnayotumia kutengeneza fufu na unga wa mihogo."

8

"Watu hupanda mashina yangu. Mifugo wenu hula majani na maganda yangu. Je, Mtende hufanya nini?" Mhogo aliuliza.

9

Mtende alicheka, akatikisa kichwa chake kisha akasema, "Mwanamke wee, unaikumbuka supu ya tende unayofurahia sana? Hutoka kwa nani?"

10

"Mimi hutoa mafuta yanayotumiwa kukaanga samaki na nyama. Je, utawezaje kutayarisha kitoweo na mchuzi bila mafuta?"

11

"Zaidi ya hayo, matawi yangu huezeka paa za vyumba vyenu na vibanda vya kupumzikia. Mnaburudika baada ya kazi kwa kuinywa kosha ninayotoa."

12

"Isitoshe, fagio zinazotumiwa kufagia vyumba na uwanja wa nyumba zenu zinatoka kwangu," Mtende alimaliza kusema.

13

"Hmmm!" Mwanamke alizusha pumzi. "Ni sawa marafiki, nimewasikia. Nitaitatua shida hii."

14

"Ninyi nyote ni viumbe muhimu sana kwangu. Pamoja, mnatengeneza mlo mtamu wa fufu na supu ya tende!" mwanamke akasema.

15

Mwanamke yule alitayarisha supu ya tende pamoja na fufu kutoka kwenye mihogo. Aliwaalika marafiki zake kula naye. Walifurahia chakula hicho sana.

Tangu wakati huo, Mhogo na Mtende wamekuwa marafiki wakubwa.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mhogo na Mtende
Author - Divine Apedo, Elizabeth Nkrumah, Georgina Abbey
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Brian Wambi
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs