Dhahabu, kalamu nzuri
Ahmed Mardiya
Andrews Opoku Antwi

Hapo zamani za kale, kulikuwa na Kijiji kilichoitwa Kalamu.

Pale kijijini, kuliishi kalamu tofauti.

1

Kwa mfano, kulikuwa na Dhahabu, Bic, Ballpoint, Gel, Marker na wengine wengi.

2

Dhahabu alikuwa msichana mrembo.

3

Bic alikuwa rafiki mkubwa wa Dhahabu.

4

Dhahabu alikuwa mwenye huzuni na wasiwasi kila wakati.

Aliishi maisha ya upweke mbali na waliompenda.

5

Hakuna yeyote aliyejua kwa nini Dhahabu alihuzunika na kuwa na wasiwasi wakati wote.

Watu waliamini kwamba alikuwa na kila sababu ya kufurahi.

6

Hata hivyo, Dhahabu alikuwa na siri kubwa ambayo yeye tu aliijua.

Je, Dhahabu alikuwa na siri gani?

7

Dhahabu alikuwa mrembo na mwenye kupendwa. Lakini, hakuwa na wino!

"Je, kalamu ya Dhahabu ina umhimu gani isipokuwa na wino?" Dhahabu aliwaelezea akilia.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Dhahabu, kalamu nzuri
Author - Ahmed Mardiya, Ibrahim Sharifa
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Andrews Opoku Antwi, Michelangelo Quaye Anang
Language - Kiswahili
Level - First sentences