Akai afurahi
Ursula Nafula
Rob Owen

Akai hakuwa na viatu.

Marafiki zake walikuwa wakivaa viatu vizuri walipocheza.

1

Akai alimwomba mamake amnunulie viatu.

Ilikuwa shida kucheza bila viatu.

2

Walipotembea kijijini, mama alitambua kuwa watoto wengine walivaa viatu isipokuwa Akai na Etabo.

3

Siku moja asubuhi, mama alimwamsha Akai.

Alimwambia ajitayarishe waende sokoni.

4

Akai na mamake walitembea hadi sokoni.

5

Walipoingia katika duka la viatu, Akai alifurahi sana.

6

Usiku ule, Akai hakuweza kulala.

Aliwazia tu viatu vyake vipya.

7

Hamu ya kuvaa viatu ilizidi.

Akai akasimama na kuvivaa viatu vyake.

8

Hata baada ya kurudi kitandani, Akai aliwaza jinsi angewaonyesha wenzake viatu vyake.

9

Akai aliamka tena na kuvivaa viatu vyake vipya.

Alicheza chumbani.

10

Mama alimpata Akai amelala kitandani akiwa amevaa viatu.

Alimwambia Akai asivivae tena viatu vyake kitandani.

11

Akai alifurahi kupata viatu kwa mara ya kwanza.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Akai afurahi
Author - Ursula Nafula
Translation - Translators without Borders
Illustration - Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - First sentences