Adie na Adhoch
Christine Nyangate
Alice Toich

Hapo zamani za kale, palikuwa na mwanamume mmoja aliyekuwa na wake wawili.

Wake zake walipata watoto wasichana wawili, Adie na Adhoch. 

Watoto hao walipendana sana.

1

Adie alikuwa mwenye bidii, mkarimu na mwenye nidhamu.

Adhoch naye alikuwa mvivu, mchoyo na mtovu wa nidhamu.

2

Adie alipendwa na walimu. Alipata zawadi nyingi kutokana na bidii yake. 

Adhoch hakupata zawadi yoyote. Mamake Adhoch alimwonea wivu Adie.

3

Mamake Adie aliugua na kufa.

Adie hakupendwa na mamake wa kambo kama alivyopendwa na mamake mzazi.

4

Adie alizifanya kazi zote za nyumbani. Hakupata nafasi ya kujitayarisha kwenda shule.

Adhoch alisoma na kucheza na wenzake.

5

Hata hivyo Adie alifanya vyema katika masomo yake shuleni. Alipita mitihani yake na kuendelea kupata zawadi.

Hili lilizidi kumkera mamake Adhoch.

6

Siku moja, mamake Adhoch alimtaka Adie aende naye kuchota maji mtoni.

Walipofika, mama alimwambia Adie achote maji safi mbali na ukingo wa mto. 

Mawimbi yalimbeba Adie hadi upande mwingine wa mto.

7

Mama aliporudi nyumbani, Adhoch alimwuliza, "Mama, Adie yuko wapi?"

Mama alisema, "Anacheza na wenzake. Atakuja nyumbani baadaye."

8

Jioni, Adhoch alienda kumtafuta dadake. Alimwita, "Adie! Uko wapi?"

Adhoch akasikia sauti ikisema, "Niko upande mwingine wa mto. Mama aliniacha."

9

Adie aliingia majini akimwita dada yake. "Adie uko wapi?"

Alisikia jibu kama lile la kwanza, "Niko upande mwingine wa mto. Mama aliniacha."

10

Adhoch aliingia majini naye akabebwa ba maji hadi upande mwingine wa mto.

11

Mamake Adhoch alikuwa na huzuni sana. Alimpoteza Adhoch kwa sababu ya wivu.

Alilazimika kuzifanya kazi zote peke yake.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Adie na Adhoch
Author - Christine Nyangate
Translation - Christine Nyangate
Illustration - Alice Toich, Catherine Groenewald, Melany Pietersen, Michael Omadi, Silva Afonso, Vusi Malindi, Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs